Enter your keyword

Culture for Life.

Monday, March 27, 2017

Dhamira alizozimulika Mwanamziki Ney wa Mitego katika wimbo wa "WAPO"


 

 Mwanamuziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki,

Dhamira zilizopo  katika wimbo wa msanii Ney wa mitego wapo
Napenda kutoa pongezi zangu kwa Raisi wetu Dkt..John Pombe Magufuli kwa kuruhusu huu wimbo kupigwa katika vyombo vya habari vilevile kumtaka msanii huyu kuongeza maudhui mengine katika wimbo huu ili kuielimisha jamii,Pili pongezi zangu ziende kwa msanii huyu wa mziki wa kizazi kipya  Ney wa mitego kwanza kabisa kwa kutumia lugha ya Kiswahili katika wimbo wake kwani unasaidia sana kuikuza lugha ya Kiswahili pia kwa kutumia lugha raihisi ambayo inaeleweka kwa jamii.

Msanii ni kioo cha jamii na ni daraja la jamii,Katika wimbo huu binafsi amenigusa sana kwani wasanii wengi wamejikita katika maudhui ya mapenzi na kusahau matatizo yanayoikabili jamii vilevile ni mfano wa kuigwa kwa wasanii wengine pamoja na kuwa fundisho kwa wasanii wengi kuwa wabunifu zaidi katika uwasilishaji wa maudhui ya wazingatie zaidi kipengele cha fani ili kiende sanjari na maudhui.

Kwa ujumla msanii Ney wa Mitego ameweka wazi matatizo yaliyopo katika jamii katka nchi nyingi.Nikianza na maudhui nita zitaja dhamira ndogondogo zilizojitokeza katika wimbo huu

       i.            Kufanya kazi kwa bidii,” uchopanda leo ndiyo utakachovuna kesho”.

     ii.            Matumizi ya madawa ya kulevya na ukabaji,mfano wasanii mateja,wanafunzi vyuo vikuu na viongozi wanaotumia madawa ya kulevya.

  iii.            Uhuru wa kuzungumza mf vyombo vya habari

  iv.            Suala la uwajibikaji kwa viongozii

     v.            Suala elimu mf kutumia vyeti bandia

  vi.            Mmomonyoko wa maadili mf  {mademu } wanawake kusagana,Biashara ya ngono,mambo hayo yapo kinyume na utamaduni wetu na si kwa wanawake tu bali hata wanaume wanaojihusisha na ushoga ni vema kuacha na kuzingatia maadili.

vii.            Mila na desturi potofu mf wasanii kulogana,wanaume kulelewa

Nay wa Mitego baada ya kuachiliwa huru



No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu