Enter your keyword

Culture for Life.

Thursday, May 21, 2015

JINSI YA KUPANGA MIKAKATI BORA KATIKA FAMILIA YAKO.




Leo katika safu hii ya maisha na mahusiano naomba tukumbushane haya,Katika jamii zetu tunaona kila siku matatizo wanayo kumbana nayo wanawake wajane.Mwanaume kumbuka wewe ndiyo msingi au kichwa cha familia,Hivyo basi kama mwanaume yakupasa kutafakari na kufanya haya katika familia yako.
  1. Mfanye mke kuwa mrithi wa mali zako.Pia hakikisha umemwandika mkeo katika nyaraka za urithi wa mali zako.
  2. Mke wako anapaswa kufahamu miradi yako
  3. Hakikisha mali zenu zina majina yenu wawili au ya watoto.
  4. Mwanaume ufanye kazi kwa bidii ili kuweza kulea familia yako.
  5. Uwe na mapenzi ya dhati kwa mkeo na kutokukubali watu,ndugu na marafiki kuwa tenganisha.
  6. Wapende wanao na kuwapeleka shule  ili baadaye waweze kujitegemea na walee katika maadili mema ya dini.
  7. Kuwa mwaminifu kwa mkeo.
  8. Kutomsema mkeo vibaya kwa ndugu na jamaa zako,Msifie mkeo kwa ndugu na jamaa na kutosema udhaifu wake.
  9. Kuwa na akaunti moja wewe na mkeo.
  10. Mkeo mpe uwezo wa kufanya kazi na kuweza kujitegemea .

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu