Enter your keyword

Culture for Life.

Thursday, May 21, 2015

Jinsi ya Kuuteka Upendo Wa Mama Mkwe.


Wanawake wenzangu wengi wetu tumekuwa tukiwachukia wakwe zetu kwa kauli za kusikia tu kwa watu.Tabia za wakwe zetu kweli huwa hazilingani wapo wenye upendo wa dhati lakini wengine utajuta hata mume utamkimbia.Leo naomba tusaidiane kidogo ili kuweza kuifurahia ndoa yako pamoja na kumpenda mkwe wako zaidi kwa vitu vidogo ambavyo havina gharama lakini vitakupa heshima na kupendwa na mama mkwe.
  1. Jifunye kunyenyekea kwa mama mkwe kwa lolote unalifanya juu yake au wewe unapo kuwa naye.
  2. Mama mkwe muone kama mama yako mzazi.Mpende kama mama yako aliyekuzaa na kuwa wazi kwake.Jitahidi kumjua kuwa anapenda nini? ili unapoweza unamnunulia na kumpa.
  3. Msifie mumeo mbele kwake,pia mwambia jinsi gani una mpenda mmeo,siyo kumpa lawama na madhaifu ya mumeo.Mambo mengine mnasuluhisha wenyewe siyo lazima kuyafikisha kwa ndugu.
  4. Si vema kuishi nyumba moja na mama mkwe kama si lazima ili kuepuka lawama na ugomvi usio na tija.
  5. Usimwite mume wako jina lake mbele ya mkweo.Itaonesha kuwa unamdharau.
  6. Tumia fedha vizuri ukiwa unaishi na mama mkwe nyumba moja pamoja na kuwa mwangalifu jinsi unavyoshi na mumeo,epuka vitendo ambavyo ni chukizo kwa mama mkwe.
  7. Penda kumzawadia unapokuwa naye hata unapokwenda kumtembelea.
  8. Mfanyie vitu ambavyo hata mama yako mzazi hujawahi mfanyia mridhishe nakumfurahia kwa yale mema anyofanya hata kama machache.
  9. Jifunze kusamehe na kusahau pale anapokukosea.Pia mtumaini Mungu sana siku zote za maisha yako.
  10. Muoneshe upendo siku zote.Nitumaini langu kuwa umeelewa ,tafadhari toa maoni yako,pia mshirikishe mwanamke mwenzio juu ya hii mada ili iwe msaada kwa wengi.Toa maoni yako hapo chini......Usisite kutoa comment zako itasaidia wengine pia.

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu