Enter your keyword

Sinyati Blog

Culture for Life.

Tuesday, September 22, 2020

FASIHI ANDISHI-KWA KIDATO CHA TATU NA NNE.

By On September 22, 2020

Mwalimu wa Kiswahili

1.Fasihi hubeba yote anayoibusha binadamu katika maisha yake ya kila siku.Jadili kauli hii kwa mifano- Maudhui (Dhamira)

2.Fasihi hubeba yote anayoibusha binadamu katika maisha yake ya kila siku.Jadili kauli hii kwa mifano- Maudhui (Dhamira)

3.Jadili vipengele viwili vya fani na vitatu vya maudhui vilivyojadiliwa katika riwaya uliyosoma.(Fani na maudhui)

4.Ujumbe wa Tamthiliya ya Kilio chetu na Orodha una umuhimu mkubwa katika Tanzania ya leo.Jadili kauli hii kwa kutumia vitabu hivyo vilivyotajwa.Maudhui (Ujumbe)

5.Taswira ni kipengele muhimu sana kwani huipamba lugha ya ushairi na kufikisha ujumbe kwa hadhira .Onesha ukweli wa kauli hii kwa kutumia vitabu viwili ya ushairi ulivyosoma kati ya vilivyosoma kati ya vilivyoorodheshwa hapo juu. Fani ( Taswira ilivyoibua ujumbe)

6.Jadili kufaulu na kutofaulu kifani kwa waandishi wa vitabu viwili vya riwaya ulivyosoma.(Fani kwa ujumla kufaulu na kutofaulu)

7.Kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma chagua wahusika watatu kwa kila kitabu na uoneshe jinsi wahusika wanavyopaswa kulaumiwa na jamii.Wahusika (dhamira au ujumbe mbaya/wasifu mbaya)

8.Kwa kutumia diwani mbili ulizosoma, eleza jinsi taswira tatu kutoka katika kila diwani zilivyotumiwa na msanii kuwasilisha ujumbe kwa jamii.Fani (Taswira zilivyoibua ujumbe)

9“Waandishi wa kazi za fasihi huibua migogoro mbalimbali na kupendekeza suluhisho ili kuelimisha jamii husika”. Thibitisha kauli hiyo kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.Maudhui(Migogoro ilivyoibua ujumbe)

10.Kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma, fafanua madhara yanayotokana na kukosekana kwa elimu ya jinsia kwa vijana kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila kitabu.Maudhui (Madhara ya usefu wa elimu ya kijinsia)

11.Jadili namna jina la kitabu la mwandishi wa tamthilia uliyosoma linavyoweza kubeba wazo kuu la mwandishi wa kazi ya fasihi.(Swali linaweza kulenga riwaya,mashairi na tamthiliya) Fani (Fafanua ujumbe uliopo katika jina la kitabu)

12.Jadili matumizi ya jazanda yalivyojitokeza katika tamthiliya uliyosoma.(swali hili linaweza lulenga  riwaya na mashairi/diwani) Fani ( Taswira)

13.Kwa kutumia riwaya uliyosoma, fafanua jinsi mwandishi alivyoweza kuwatumia wahusika wawili katika kuibua maudhui yake.Fani (Wahusika na maudhui( ujumbe,dhamira,migogoro)

14.Tumia Riwaya ulizosoma kisha toa hoja tano (5) zinazo thibitisha kuwa wanaume ni kikwazo cha mafaniko katika jamii. Maudhui( nafasi mbaya ya mwanaume)

15.“Kazi za fasihi hufichua mivutano/mitafaruku  iliyopo katika jamii” kwa kutumia hoja sita (6) kutoka diwani mbili ulizosoma darasani .Fafanua mivutano hiyo hoja tatu kutoka katika kila diwani.Maudhui (migogoro)

16.“Kipenda roho hula nyama mbichi”.Fafanua msemo huu kutoka riwaya ya Takadini na riwaya ya Watoto wa Mama n’tilie. Kwa kutumia hoja sita(6) Maudhui (Mambo hasi yaliyotokea kwa wahusika kutokana na matendo yao)

17.Waandishi wengi wa tamthiliya wanajitahidi kuonesha ufundi wao kwa kutumia tamathali za semi mbalimbali katika kazi zao.Thibitisha ukweli wa kauli hiyo kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma darasani.Hoja (3) kutoka katika kila tamthiliya.Fani (Tamathali za semi)

18.Waandishi wa kazi za fasihi andishi  huandika kazi zao kulingana na jina la Kitabu jinsi lilivyo.Kwa kutumia  hoja tatu kutoka kila tamthiliya onesha namna jina la kitabu linavyoendana/kusadifu mawazo ya mwandishi.Fani (Fafanua ujumbe uliopo katika jina la kitabu)

19. Kwa kutumia riwaya mbili ulizosoma fafanua namna ambavyo waandishi wametumia kipengele cha mtindo kuumba kazi zao.Toa  hoja tatu kwa kila kitabu.Fani (Mtindo)

20.Kazi za fasihi andishi zinafananishwa na kisu kikali katika jamii zetu” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa vitabu viwili ulivyosoma.Maudhui (Ujumbe)

21.“Mshairi siku zote hukemea uonevu katika jamii”Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.Maudhui (dhamira)

22.“Fasihi ni chuo cha kufundisha maisha kwa jamii husika” Jadili ukweli wa kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila riwaya mbili ulizosoma.Maudhui (Ujumbe)

23.Kwa kutumia hoja tatu kwa kila tamthiliya mbili ulizosoma,jadili kufaulu kwa waandishi katika kipengele cha utumizi wa tamathali za semi.Fani (Kufaulu kwa matumizi ya tamathali za semi)

24.Msanii ni kinda la jamii husika,hivyo anayoyaandika ni kuhusu jamii hiyo. Jadili kauli hii kwa kutumia hoja tatu(3) kutoka katika kila diwani moja kati ya diwani mbili ulizosoma.Maudhui (Dhamira)

25.Jadili wahusika wawili kama kielelezo halisi cha kukubalika au kutokukubalika kwao katika jamii kati ya Takadini,Mamantilie na Brown Kwacha kutoka katika riwaya mnili ulizosoma. Fani (Wahusika)

26.Dhana ya mapenzi imejadiliwa  kwa mapana .Thibitisha kauli hii kwa kutumia tamthiliya kati ya ulizosoma. Maudhui (Mapenzi ya dhati na yasiyo ya dhati)
Kujikomboa ni kwa namna nyingi katika maisha ya mwanadamu.Thibitisha kauli hii kwa mifano kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.Toa hoja tatu kwa kila kitabu.Maudhui (ukombozi)

27.

Saturday, August 8, 2020

Chupa ya Wine Inapokuwa Pambo la Nyumba yako.

By On August 08, 2020

 


Chupa ya wine hutumika kama pambo la nyumba
Add caption

Chupa hii nimeitengeneza mwenye kwa kutumia spray print kama utapenda usisite kunitafuta kwa email yangu au namba 0756377940

Mpenzi msomaji wa makala hii  ni wazi kuwa uko poa mbali na janga hili la Corona wewe unaendelea vema.Leo napenda nikushirikishe jambo moja namna ya kubadili taka kuwa pambo.Kwanini nasema taka,kwasababu wengi wetu hutupa chupa za wine ,shampeni na chupa zingine kwasababu hazina kazi tena.

Leo nitakupa mbinu kazaa za kupendezesha nyumba yako kwa chupa ulioitumia na utaacha kutupa kabisa wakati mwingine.Nitakudokeza vitu vichache unavyopaswa kuwa navyo ili uweze kutengeneza chupa ya na kuipa muonekano mpya.

Chupa ya wine au shampeni

Add caption

Rangi (Spray paint)

Zipo nyingi maduka ya hardware ni kiasi cha kuchagua wewe unapenda nini?

Namna ya kujifunza zaidi pitia youtube by Ayo craftt ( Namna ya kupamba chupa yako kwa spray paint)



Wednesday, December 4, 2019

Dhima za viambishi.

By On December 04, 2019

Wednesday, April 10, 2019

Umuhimu wa wazo katika Ubunifu . .#Afriposhdesign #Tanzania culture

By On April 10, 2019

Wasifu Binafsi
Jina -Glory James
Primary-Nkoanrua P.School
Secondary-Nkoanrua S.School
Univerisity-SUA
Wazo lako ndiyo utajiri wa maisha yako,Mtu mwingine hawezi kujua mawazo yako zaidi ya wewe mwenyewe utakapo lifanyia kazi wazo lako.Marafiki, wazazi,ndugu na watu wanao kuzunguka hawezi kuona faida ya wazo ikiwa wewe mwenyewe huwezi kulifanyia kazi ili waweze kuliona.

Safari ya Binti  Glory katika tasinia ya ubunifu
Amesomea mambo ya kilimo lakini aliona vema kutumia kipaji chake badala ya kuajiliwa.Afriposhi ilifanikiwa alipoamua kufanya na kuhakikishia umma kuwa inawezekana kufanya kazi za mikono bila kusita na kusubiri ajira .Anasema"Wazazi wangu hawakupenda nijiajiri lakini nilipowashilikisha na kuonesha juhudi, mama yangu alianza kunisaidia,na biashara yangu nafanya kupitia mindao ya kijamii hasa Instagram,Kupitia Instagram napata wateja wengi kutoka n'je na kidogo ndani ya nchi" Mpaka sasa ana followers 30.9k





Watanzania wengi hawajui namna ya kuvaa mapambo ya kiutamaduni(accesories) na mavazi yao jambo ambalo linapelekea kukosa wateja wa ndani.Wengi huamini kuwa vitu vya utamaduni vinafaa kuvaliwa na nguo za kitamaduni kitu ambacho sio sahihi kabisa.Vazi lolote linaweza kuvaliwa na culture yoyote ilimradi uzingatie muktadha(Location)

Changamoto anazokumbana nazo kubwa ni soko la ndani kutofahamu umuhimu wa vitu vya ndani na kujua namna ya kuvitumia hivyo ina mrudisha nyuma kibiashara na kujikita na soko la n'je.Wakati mwingine huwa inambidi kufundisha watu namna ya kuvaa na nguo.

Ushauri wangu kwa mabinti ni kuweza kuyafanyia kazi mawazo yao na kuacha kubweteka kwani linapoanza wazo moja huzaliwa wazo lengine.


Amekwisha valisha wasanii kama:Jokate Mwegelo na Janethn Jackson n.k
kwa maelezo zaid mfollow instagram: #Afriposhdesigns.  #Afriposhdesign or Glory
Anapatikana Arusha viwanja vya nanenane.
Phone no.0757074590,0756377940

Wednesday, February 20, 2019

African Necklace/Mikufu ya Shanga

By On February 20, 2019
Penda kujivunia utamaduni wako.Vitu vya asili kama mavazi ,vyombo,nyumba zilizojengwa kwa ubinifu wa hali ya juu lakini muonekano ni waasili pia huvutia sana.Leo nataka kukupa siri unapovaa vazi la asili na vikorombwezo vyake huwa ina pendeza na kukupa muonekano wa tofauti sana.Kitu unachopaswa kufahamu unavalia nini na kwa wakati gani?
Ukitaka kupendeza na culture vaa na nguo  ya rangi moja ili urembo uonekane.



120,000/=


Hii baadhi ya mikufu iliyotengenezwa kwa shanga na nyuzi.Endapo utapenda usisite kunipigia kwa mahitaji zaidi pia tuna valisha mtu anayetaka kuvaa kiasili katika matukio yoyote.Nicheki inta kwa jina la sinyatiblog na whatsapp 0756377940.
100,000/=


65,000/=

45,000/=

100,000/=


120,000/=

Sunday, January 13, 2019

Colar Living Rangi ya mwaka 2019#Coral Living

By On January 13, 2019




              Optimism colar living color of the year 2019





Coral Living  ni rangi iliyochaguliwa na kampuni ya Pantone  rangi imeonesha kuvutia na viumbe wanaoishi kwenye maji,na hii rangi huwa inapatikana kwenye coral reefs,mwaka huu inabeba ujumbe kuwa ni rangi yenye kuonesha matumaini,ujasiri na mafanikio katika mwaka 2019.


Kama uliweza kufuatilia rangi hii ilitumika sana katika nyumba,ambapo watu wengi walikuwa wakipatka rangi hii kwenye kuta za n'je.turajie kuiona rangi hii katika sherehe nyingi.Ingawa wakati mwingine huwa si lazima kuitumia rangi ya mwaka inategemea na upendeleo wa Mtu wa rangi.
Nanukuu:






"Pantone Color of the Year 2019 Mug

SKU: 2019-001


Pair your favorite hot beverage with the cool new Color of the Year 2019: PANTONE 16-1546 Living Coral

The Pantone Color of the Year 2019, PANTONE 16-1546 Living Coral is an animating and life-affirming shade of orange with a golden undertone. We get energy from nature. Just as coral reefs are a source of sustenance and shelter to sea life, vibrant yet mellow PANTONE 16-1546 Living Coral embraces us with warmth and nourishment to provide comfort and buoyancy in our continually shifting environment"

Heshima ya Mwanamke katika harusi na send-off

By On January 13, 2019
Mwanamke unavaa vazi kama hili.Matiti yote yako n'je tubadilike

Utamaduni wetu pamoja na maadili ya dini miaka ya nyuma mwanamke alikuwa anajistili vema kwa kuficha maungo yake lakini sasa hivi wanawake tunaanika sana viungo vyeti vya mwili bila kujali kupoteza haiba zetu.

Binti anapoolewa au anapokuwa katika sherehe yoyote wengi wetu siku hizi zimekuwa kama sehemu za kuonesha miili yetu,wengine ni sehemu ya kutafutia wachumba.Naenda kusema kuwa mwanaume atayevutiwa na mwili wako kwa kuuonesha huyo utakuwa kakutamani hajakupenda.Mume wa kukuoa aangalii hivyo vitu unavyomuwekea n'je.

Leo napenda kugusia kidogo suala LA wanawake wanao ingia katika ndoa.Tunajua kuwa siku ya harusi,kitchen party,sendoff na sherehe zingine wewe kama mwanamke usisahau maadili ya utamaduni wako na dini pia,Wanawake siku hizi mavazi yao yamekuwa ya kuacha miili yao wazi  najiuliza unamuonesha nani?au ndo mitindo ya nguo siku hizi lkn neno moja ni kwamba unajidharirisha.

Monday, August 13, 2018

Mishono mipya ya sendoff Agosti 2018.#vitenge

By On August 13, 2018
Binti unayeagwa ni vema basi kuwa angala na mavazi ya kanisani, wakati wa kupiga picha,nyumbani, na vazi la kuvaa ukumbini kama una uwezo wa kufanya hivyo lakini kama huna mavazi mawili tu yanakutosha.

Vazi la kanisani ndilo utakalokwenda nalo kupiga picha kisha ukimaliza utaenda kuagwa nyumbani na familia yako.Kisha ukumbini unatafuta vazi zuri litakalo kufaa.

Kumbuka kuwa ugumu wa maisha au ukubwa na udogo wa mambo uko juu yako kulingana na kipato chako.

Baadhi ya picha zilizo nivutia katika muonekano wa vazi la Sendoff:








Furaha ya Wazazi ni kumuaga binti yao #Sendoff Party#Mishono ya Sendoff

By On August 13, 2018
Ushawahi kujiuliza  haya maswali,kuwa ni rangi gani utavaa wakati kuagwa nyumbani kwenu,Ushawahi jiuliza unataka kuwa na muonekano gani siku ya sendoff yako,Je?Mume wangu mtarajiwa atavaa nini? ni kweli ni lazima tufanane kimavazi hata rangi tu ya nguo ina ulazima gani?,Wageni waalikwa watavaaje katika siku yangu.

Binti unayeagwa ni vema basi kuwa angala na mavazi ya kanisani, wakati wa kupiga picha,nyumbani, na vazi la kuvaa ukumbini kama una uwezo wa kufanya hivyo lakini kama huna mavazi mawili tu yanakutosha.

Vazi la kanisani ndilo utakalokwenda nalo kupiga picha kisha ukimaliza utaenda kuagwa nyumbani na familia yako.Kisha ukumbini unatafuta vazi zuri litakalo kufaa.

Kumbuka kuwa ugumu wa maisha au ukubwa na udogo wa mambo uko juu yako kulingana na kipato chako.
 
Baadhi ya picha zilizo nivutia katika muonekano wa vazi la Sendoff:



Kwa maelezo zaidi tafuta ukurasa wa  mwanamitindo

Tuesday, May 22, 2018

Bold fashion

By On May 22, 2018
 Socks with heels is a bold fashion statement that we have seen on most and popular bloggers who have bold and adventurous style, but that doesn’t mean you can’t absolutely rock that trend, too. If you think that classic pumps and sandals too formal for street wear, then wear socks with them to make it cool and more casual.






You can wear quirky socks and shoes combo in different contrasting shades, or wear a quirky ensemble in your outfit like a skirt, blouse, dress, or even accessories. When wearing statement socks and shoes combos, always play it safe with the rest of your outfit and keep it simple and polished. And when wearing more colourful outfits with different patterns – opt for a neutral combination of your socks-and-shoes to balance it out.
Print from @gtp_fashion
Outfit designed by @madlynmodegh
Hair from @neweditiontrendz
Laid and styled by @kukispalour
Shot by @ansahkenphotography
source:www.akosuavee.com/bold-fashion/

Monday, May 21, 2018

Harusi itakayofunga mwaka 2018#Meghan Markle &Prince Harry.

By On May 21, 2018
Ilikuwa tarehe 19 mei 2018.Ambapo Prince Harry na Meghan Markle waliweza kufunga ndoa  katika kanisa la St.George's Chapel Windsor caster-United kingdom.

Inasadikika kuwa watu million 18 nchini marekani na watu milioni 100 duniani waliweza kuitazama harusi hiyo kupitia vyombo vya habari vilivyokuwa vina rusha harusi hiyo Mubashara.Ilirushwa  kupitia CNN,BBC America,Sky News,Fox ,BBC one.na vingine vingi.

Meghan Markle akiingia kanisani,picha ya kushoto na kulia akiwa amevaa gauni  la reception.
Prince Harry akiwa na masimamizi wake(best man)

Prince Harry na mkewe Meghan Markle.wawili hawa walianza mahusiano tangu 2016,Meghan (ana umri wa miaka 36)alishawahi kuwa mwigizaji nchini marekani ameigiza filamu kama Get him to the Greek,Horrible Bosses na uhusika wake wa kwanza katika kuigiza ulikuwa Nesi kwa Mara ya kwanza kabisa.
Meghan aliacha kuigiza baada ya kuvalishwa Pete ya ndoa  mnamo tarehe 27 Novemba 2017

Meghan katika uasilia wake, katika harusi nyingi za kibongo watu hujisiriba mapambo usoni na kuondoa uasilia wake ambao Mungu kakupa na Mume akaupenda.Ningeomba Muige huu mfano.


Saturday, May 12, 2018

Hii ndiyo rangi ya mwaka 2018#purple

By On May 12, 2018
Kumekuwa na mkanganyiko sana kuhusu rangi ya mwaka,Wengine wamekuwa wakidai bluu ndiyo rangi ya mwaka kutokana na kwamba mwaka Jana ilivaliwa mno hasa na maharusi.

Naomba nikutoe kimasomaso rangi iliyotangazwa na Pantone ambayo ninkampuni inayotekeleza jukumu hilo baada ya kufanya utafiti katika mitindo mbali mbali hutoa rangi ya mwaka.

Rangi ya dhambarau IPO katika muonekano tofauti .nitatupia picha chache za mavazi ya rangi ya purple( zambarau)






Friday, May 11, 2018

Ubunifu wa kipekee,kwa mtu wa kipekee

By On May 11, 2018



Ninapozungumzia ubunifu,hii ni hali ya kuwa na wazo La tofauti katika jambo unalofanya,Mimi nazungumzia ubunifu wa mavazi ambao humfanya mtu kuwa wa kipekee.

Hivyo upekee wa mavazi ndiyo hutambulisha mtu,mfano mtu huambiwa umevaa kama changudoa kutokana na muonekano wa vazi hulilovaa kuwa ni la kichangudoa,au unaweza ambiwa umevaa kama bibi,babu,kijana,mshamba ,miss nikutokana na muonekano wako.

Ushauri wangu ningwomba uwe na mtindo wa vazi lenye staha linalokutambulisha vema.

Wednesday, April 18, 2018

Vazi la Ubunifu kwa kutumia Ungo#Makeke

By On April 18, 2018
Baada ya uzoefu mkubwa katika matumizi ya mapishi jikoni, ungo umejizolea umaarufu mkubwa  baada ya kuingizwa rasmi katika tasnia ya sanaa hususani katika  ubunifu wa mavazi na kupewa jina la *LUPAHERO* na Jo;cktan Makeke.
 *MAANA YA LUPAHERO*


Ubunifu huu wa mavazi umepewa jina la *LUPAHERO* ambalo ni mchanganyiko wa majina mawili ambayo ni *LUPAPIKE*, neno la *kinyakyusa* lenye maana ya ungo na neno la pili ni *LUHELO*, ambalo ni neno la kihehe lenye maana ya ungo.
Muunganiko wa maneno haya mawili umelenga kuleta dhana ya ushujaa kutokana na ladha ya mavazi hayo kuwa na dhima hiyo, huku neno Luhelo likitamkwa herufi za mwisho kama Hero, herufi *L* ikibadilishwa kuwa *R* ili kupata neno *hero* la kingereza lenye maana ya shujaa na kukamilisha maana halisi ya ubunifu huo kuwa shujaa wa ungo.


Thursday, March 29, 2018

Kitenge ndani ya Manyoa.#kichenparty#vitenge

By On March 29, 2018
Tunapozungumzia ubunifu,ni ufundi anaoutumia msanii yeyote katika kuwasilisha/kufanya kazi yake iwe tofauti na na kazi za watu wengin

Vazi La kitenge ni vazi unaloweza kuchanganya na kitambaa au mapambo yoyote katika ubunifu na ukapata vazi LA kipekee ,kama hilo vazi ni la kitenge ila limetiwa nakshi za manyoa kazi kwako.

Saturday, March 10, 2018

African kids Fashion#2018

By On March 10, 2018

Watoto wadogo  siyo lazima kuwanunulia mavazi ya special ama mtumba wanaweza kupendeza katika vazi LA kiafrika na wakawa na muonekano mzuri.Kama unavyoona  baadhi ya hawa watoto wakiwa katika mavazi ya mutadha tofauti.

Watoto katika vazi la Nigeria

 Kivazi cha part kwa mtoto(baby yellow)
 Katika muonekano wa vazi la kibunifu la kitenge kipart zaidi.


3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu