Enter your keyword

Culture for Life.

Tuesday, May 23, 2017

Beyonce Baby Shower #ASili ya Baby shower na namna ya kuifanya.

By On May 23, 2017
" Baby shower"Asili yake ni kwamba hufanya mwanamke mjamzito,mimba yake inatakiwa iwe na miezi sita(6) au nane(8) na kwautamaduni wa wenzetu kama Egpty ufanya hasa kwa mwanamke ambaye anatarajia kupata mtoto wa kwanza katika familia yake.Pia kipindi hiki mwanamke anatakiwa kula milo mizuri kwa ajili ya kujenga afya ya mtoto.

Ambapo mwanamke huyo huwaalika rafiki zake wa kike ambao humletea zawadi za mtoto,Hii pia humsaidia mwanamke kujiandaa kuwa mama mwema na kujua mavazi ya kumvisha mtoto pamoja na kumlea,Vilevile unaweza kufanya baby shower kwa mtoto ambaye anajinsia tofauti na yule wa kwanza.

Pia baba wa mtoto anaweza kufanya baby shower ambapo anaweza kuwaalika wanaume wenzake na wakampa zawadi za mtoto,anaweza kufanyia sherehe hizo pub au sehemu nyingine ambapo wanaweza kunywa,kuangalia mpira na kufanya mambo mengine ambayo wanaume wanaweza fanya wanapokuwa pamoja.

 Vilevile mwanamke huweza kuweka mchezo wakati wa kufungua zawadi ,hii pia husherehesha sherehe.




 Katika party aliyooita  "Carter Push Party’ and Twinning" pia wanawake maarufu walioweza kuhudhuria siku hiyo kama... star Serena Williams,La La Anthony,Kelly Rowland and Michelle Williams,
Sherehe zingine ambazo zinaweza kufanya ni pamoja na Diaper Shower,Grandma's Shower,Sprinkles shower.

Monday, May 22, 2017

Muoekano mzuri wa kwenda beach kiutamaduni zaidi

By On May 22, 2017
Kujivunia vitu vya asili ni muhimu kwa kila mwananchi bila kujali utaifa wako.Leo nitaongelea ubebaji wa mikoba ya asili wakati unapokwenda kupumzika ufukweni na familia yako,marafiki au mpenzi wako.Basi vitu vyako unaweza weka katika mikoba hii,pia hakikisha unavaa viatu flat kama ambavyo vinaonekana hapo.



Sunday, May 14, 2017

Pleated skirt # Skirt za malinda zimerudi tena katika mitindo ya mavazi.

By On May 14, 2017
Malinda katika vazi la mwanamke yalionekana sana katika mavazi ya wanafunzi hasa mashuleni lakini miaka 1994 mavazi yenye mtindo huu wa malinda yalivaliwa sana na wamama(wakina mama wenye makamo)vilevile mavazi yenye malinda yalivaliwa sana na watoto wa kike,hasa katika magauni au skirt zao .


Sasa hivi hili vazi linavaliwa na kinadada zaidi,lakini hata msanii wa kike Emilia Clarke katika filamu ya Game of Throne ameonekana pia kavaa vazi hili la malinda .vazi linaonekana vema pale alipokwenda kuwafunga Dragoni wake baada ya kuua mtoto mmoja baada ya Emelia kuletewa mashitaka, aliamua kuwafunga hao Dragoni kwa minyororo .Basi katika onesho hilo utaona vema vazi hili la malinda katika gauni la mwanadada huyu mwenye umri wa miaka 31 sasa.


Emelia Clarke katika gauni lenye malinda,Amezaliwa 23/10/1986

Mitindo ya skirt za wanawake kwajili ya kanisani.

By On May 14, 2017
Wanawake tumeumbwa kuwa walezi katika ulimwengu huu,Hivyo hata vazi la mwanamke linapaswa kuwa la mfano katika nyumba ya ibada,Mwanamke unapokwenda kanisani hakikisha unavaa vazi ambalo halioneshi mwili wako.Mwanamke katika kanisa ni muombolezaji katika kuombea kanisa.






Sunday, May 7, 2017

women# Uzuri wa Mwanamke wa Kiafrika upo Katika uwezo wake:

By On May 07, 2017
Nimevutiwa na hu ubunifu wa Kitambaa kilichofungwa kichwani hapo ni vitenge vya aina mbili tofauti,Katupia na short jumpsuit na accesories....Kama umependa unaweza tupi kichwa kilemba cha kitenge lakini simple sio furushi lote hilo kwa mtoko zaidi.

Tuesday, May 2, 2017

Men# Mwanaume ni pambo la mwanamke.

By On May 02, 2017
JOHN- DUMELO ni msanii  katika tasnia ya filamu toka ghana namkubali kwani miongoni mwa wanaume watanashati ambao kiukweli muonekano wao unanivutia sana ni mpambanaji na anaipenda jamii kwa ujumla.Tuzo alizowahi kupata..
Nollywood Movie Award for Best Actor in a Supporting Role
2012 · A Private Storm
Africa Movie Academy Award for Best Actor in a Supporting Role
2011 · A Private Storm
Africa Movie Academy Award for Most Promising Actor
2010 · Heart of Men
City People Entertainment Award for Best Actor of the Year (Ghana)
2016, 2014
City People Entertainment Award for Best Supporting Actor of the Year (Ghana)
2016


Leo nitakupa siri moja yaani jinsi ambavyo wanawake  tunavutiwa  na wanaume nadhifu, basi hata sisi wanawake tunavutiwa na wanaume wasafi kuanzia muonekano wake,Jinsi anavyoipenda ngozi yake,usafi wa mwanaume si tu kuoga maana wanaume wengine kuoga kwao mpaka sherehe,Unakuta mwanaume ananuka kikwapa yaani akikusogelea unatamani ukimbie hata kuongea naye ndiyo noma zaidi mdomo unanuka usipime.

Mwanaume mtanashati ni yule aliyevizuri katika fikra zake,mipango yake iko vema,Anajikubali na cha zaidi mwanaume asifiwi usafi tu hata kipato na ujue kutunza familia yako nyumbani pamoja na kuwa na mchango mzuri kwa jamii yako.

Mwanaume ambaye hakumbuki boksa yake alifua lini au aliibadilisha lini mmmh huyo hata mwenzi wako atakosa hamu na wewe maana mnapokutana anajua tu huyu mtu ndani yukoje?

Mwanaume anayenuka miguu wala hakumbuki kucha za miguu au mikononi alikata lini mhh huyo si mtanashati,
 Mwanaume anayejua kupangilia mavazi yake huyo nikivutio cha wengi lakini si mwanaume anayevaa kiuhuni,Hata kuaminika si rahisi sana,haijalishi unafanya kazi gani jiweke nadhifu.
Mwanaume asiyejua kuchana nywele au kutambua mtondo gani wa nywele akinyoa una mpa muonekano mzuri mmhmm.
 Mwanaume ambaye nyumba yake ipo katika mpangilio mbaya yaaani sebuleni ndoo za maji katikatiya meza,kitanda shuka la rangi ya kuficha uchafu au hakitandikwi wala mashuka haya fuliwi mmhm,,, 

Mwanaume ambaye ajui kupaka mafuta ,wala hajui thamani ya ngozi yake mmmh  hapana si mtanashati,na hajali ngozi yake huyo hapana maana akifungua vifungo vya shati lake au kuinua suruali yake miguuni yaani ngozi haifai haina hata mvuto dthh no.

 Nitaongea machache tu leo, siku nyingine nitaongezea. Jua tu mwanaume pia ni pambo la mwanamke hatuvutiwi na wanaume wachafu Na kama ukiona umependwa na wala huyo uliye naye hakuweki smart jua kuna kitu kafuata kama si pesa basi kingine{...................}

Mwanaume yeyote unayesoma makala hii kama unatabia moja wapo au ambazo sijazitaja unaweza jirekebisha,lakini kama unaona kuna tabia ambayo sijaitaja unaweza ongezea hapo na nitaiongeza katika makala hii...(COMMENT NI KWA JINSIA ZOTE UNAWEZA COMMENT)

MEN SWEATERS# Aina ya masweta ambayo mwanaume unayopaswa kuvaa ofisini

By On May 02, 2017

Nitadokeza aina ya masweta ambayo ukivaa kazini yatakufanya uonekane nadhifu:



Vesti sweta,Haya ni masweta ambayo ukikosea tu kuchagua unaweza kuonekana mzee au sweta likaonekana la mtoko,chagua Rangi nzuri kwa ofisi ni silki au nyeusi.Unaweza vaa na tai ndefu,au bow tai.

Solid-Color Sweta,Masweta ya mtindo unaweza kuvaa na  shati lenye kola yapo ya rangi tofauti lakini angalia rangi ambayo haing'ai sana rangi zilizopoa ni nzuri zaidi.Kwa mtu mfanyabiashara hupendelea rangi hizi zaidi ambazo ni nyeusi,kijani iliyoiva,maruni na grey

Argyle Sweta,Wanaume wengine hupenda masweta yenye michoro basi ukipata sweta lenye mistari kama hili  ni zuri zaidi.

Sweta za mistari,Hizi sweta ni nzuri sana lakini hakikisha kama una umbo kubwa chukua sweta zenye mistari midogo kwani huasahidia hata kufisha muonekano wa unene wako au kitambi,mtu mwembamba tumia sweta zenye mistari mikubwa zingatia pia ku match na surualia au shati lako pamoja na kiatu.
vilevile haya masweta unaweza vaa kazini ikiwa baridi ni kali sana kwani haya huwa ni mazito mno na hufaa kwa mtoko au mtaani.

haya masweta yanafahamika zaidi,unaweza vaa kama unavyoona hapo katika picha lakini siyo lazima ukunje.

Monday, May 1, 2017

Joggers for Men: How to Wear Joggers

By On May 01, 2017
Zamani sngland(jogger) zilikuwa zikivaliwa na wanaume kwa ajili ya michezo.Joga ni huwa na kitambaa kinachotanuka,pia huwa nyepesi vilevile huwa hazingizi joto.Hivyo wanaume wengi hupenda kuvalia ndani ya nguo zao kabla ya kuvaa shati au kuweka jacketi juu.Kwa ajili ya kazi ni vema kuwa na joga nyeupe ambayo hata ukivalia suti au wakati wa joto unapovaa si rahisi kupitisha joto.

Mwanamke mwenye mahaba ya dhati hapaswi kufanyiwa haya:

By On May 01, 2017
  •  
    Blogger:Sinyati,Maoni ni kwamba ni vema kuwa wa wazi na wa kweli linapotokea suala la mahusiano.Hii itasaidia watu kutokuwa na malipizi kwa walio watenda.
  • Usimuumize moyo wake
  • Usijifanye unampenda ili ufanikiwe kufanya yako.
  • Mtukane vyovyote vile ila sio wazazi wake na kumwambia kuwa yeye ni mbaya.
  • Usimfananishe na wanawake zako waliopita.
  • Usimpige,ni vema kuongea naye kwa utaratibu. Usimsaliti na kuonyesha kabisa dharau ajue kuwa unamsaliti
  • Usimvunjie heshima kwa kumgombeza mbele za watu.
  • Usimpotezee muda wake kama hauna mpango wa kumuoa, unamchelewesha kupata mume bora.
  • Usimfanye ajione hapendwi na ana mkosi hapa ulimwenguni.
  • Usimradhimishe kufanya tendo la ndoa
  • Kamwe usisahau kumwambia unampenda na yeye ni mzuri hiyo haipunguzi nguvu za kiume.
  • Usimpe mimba na kumkimbia au kumwambia aitoe, kama huna nia ya kumuoa achana na hayo

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu