Enter your keyword

Culture for Life.

Saturday, March 16, 2013

Sheria za uvaaji wa suti na Tai



Ni wazi kuwa  wengi tunalitambua vazi hili na miongoni mwetu tunapendelea kulivaa vazi hili. Suti huvaliwa na jinsia zote mbili yaani wanawake na mwanaume, isipokuwa mwanaume hawezi kuvaa suti ya sketi kama ilivyo kwa  wanawake,ambao wana uwanja mpana katika uchaguzi wa Suti. Vazi hili huvaliwa sana maofisini katika Taasisi binafsi na za serikali,kwenye harusi,sherehe,mikutano, na mazingira tofauti ambayo ni rasmi.Leo mpenzi msomaji wa safu hii Naomba tukumbushane baadhi ya kanuni za vazi hili la suti ambazo zitakupa hadhi ndani ya vazi la suti kama ifuatavyo:

1.      Epuka kuchomekea koti
2.      Epuka kutembea peku
3.      Usipende kuongea kwa sauti au kupiga kelele wakati unazungumza
4.      Acha kula magengeni.
5.      Usipende kupanda Daladala,kuendesha pikipiki au baskeli ukiwa umevaa suti
6.      Usivae kandambili au kubeba mfuko wa plastiki(Lambo)
7.      Usivae soksi zilizo chanika na suti
8.      Usijisaidie uchochoroni (kuchimba dawa) uwapo safarini.
9.      Epuka kupenga kamasi barabarani au kutema mate hovyo
10.  Acha kuchekacheka hovyo
11.  Epuka kutafuna hovyo barabarani
12.  Usitembee  na pesa za sarafu mfukoni
13.  Marufuku kupiga mruzi
14.  Marufuku kutokwa na jasho hovyo,tembea na leso
15.  Usipende kukimbia ukiwa ndani ya vazi la suti
16.  Marufuku kuwa mbishi au kusababisha mjadala usio na maana
17.  Usinywe  pombe za kienyeji wala kukaa sehemu zenye vilabu vya pombe za kienyeji


No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu