Enter your keyword

Culture for Life.

Tuesday, March 26, 2013

BORA MUME WA MTU AU MKE WA MTU

Hakuna lililo bora katika hayo yote ,
vijana wengi siku hizi huona bora kuwa na mahusiano na mtu zaidi ya mmoja au kutembea na mume wa mtu au mke wa mtu,leo nataka mpenzi msomaji utambue kitu kimoja kama mwanadamu na mwenye utu ndani ya moyo wako na ambaye baadaye unategemea kuitwa mama au baba,lile umfanyialo mwenzako leo jua kesho kwako.

Kuna ushuhuuda niliusikia kwa masikio yangu kanisani binti mmoja aliyetembea na wanaume 100 kwa mda wa mwaka mmoja akishuhudia kanisani na kati ya hao wengne ni waume za watu. Je wewe ushatembea na wangapii nitakacho kusema hapa ni kwamba tutambue kuwa kila mwanaume utakaye tembea naye anamikosi yake je kama umetembea na watu 100 ushawahi kukakaa chini na kukili hilo na kuvunja laana ambazo wanazo hao watu uliotembea nao jua kuwa laana zao ziko pia ndani yako kwasababu ulisha ungana nao.

Mpenzi msomaji mikosi mingine ni kutokana na matendo yetu kutokufanikiwa katika maisha ni kutokana na hawa watu tunao kumbana nao bila kuwajua,kama una mke kwanini usiridhike na mkeo au mumeo na kitendo cha mwanamke kuwa na mume wa mtu au mwanaume kutembea na mke wa mtu ni laana tunazozitafuta wenyewe,hivi haijawahi kukutikea umetembea na mtu leo siku hiyohiyo unakumbana na matatizo kibao au ukiwa naye matattizo haya ishi.

Ungama leo kama kijana ,mume wa mtu,au mke wa mtu acha na subiri yule ambaye mungu amekupa.Tufute mikosi na tuwe na tumaini la mafanikio kwa kujaliana wenyewe kwa wenyewe na kujijali wewe mwenyewe.

Kama uko tayari ungama na futa laana na maagano ya watu wote ulikutana nao.

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu