Enter your keyword

Culture for Life.

Saturday, January 7, 2017

Maswali 20 ya kujiuliza Kabla ya Kuingia Kwenye Ndoa.


Una mpenzi au mchumba mnapendana sana Je umewahi  kujiuliza haya maswali Kabla hujaingia kwenye ndoa?




 SARA ISSA AKIWA NA MUME WAKE.

               
Swali #1:Ni kiasi gani cha fedha tunacho na ambacho tunaweza kutumia kwa mwaka mzima au kila mwezi.                                                                                                                                                          
Swali# 2:Nani anahusika na matumizi ya nyumbani pamoja na gharama za mipango ya nyumba yetu.      

               
Swali# 3:Ni kiasi gani cha fedha tunaingiza pamoja,kwasasa,ndani ya mwaka mmoja,miaka 10 na nani anahusika kuingiza kiasi kikubwa zaidi katika malengo yetu. 
             
Swali#4:Malengo yetu ya mwaka mzima katika mapato tunayoingiza ni yapi? tutatumia jitihada zipi kufanikisha.

Swali #5:Je? gharama za matumizi yetu katika (Kodi,Bima,mavazi,chakula na usafiri)yapoje na tunatumia shilingi ngapi kwa mwezi au mwaka mzima.Tumepanga kutumia vipi?

Swali#6:Je?Mda gani ambao kila mmoja wetu atautumia kazini au tumepanga kuanza kazi mapema sana au kazi zetu ni za jioni tu.

Swali#7:Je kama mmoja wetu hataki au hawezi kufanya kazi katika mazingira yoyote yale itakuwaje? au tutafanya nini?

Swali#8:Je mwenzangu anapenda nini na je ninafurahia anachokipenda mwenzangu.

Swali#9:Nipo huru ninapokutana na mwenzangu katika tendo la ndoa,na je nalifurahia.

Swali#10:Je tunafanana katika makubaliano yetu ya kukutana kimwili,tunawezaje kumudu haja zetu kama hazifanani,kidogo  au sana labda mwenzangu anahitaji usiku tu,mchana,kwa wiki mara moja au kila siku au kwa mwezi au mwaka..

Swali#11:Je tunakula chakula pamoja na ni nani anahusika na gharama za chakula,nani anapika na kusafisha baada ya kula.

Swali#12:Je wote tuna tabia zinazofanana,mfano kunywa pombe,kuvuta sigara kula sana nk
.
Swali#13:Je familia za wenzetu zinaishije,tutakuwa tunafanya matembezi ya kuwatembelea au kuwa ruhusu kutumbelea na kwa kipindi gani?

Swali#14:Tutakapopata watoto je ni mahusiano gani tutayaruhusu kati yao na bibi au babu kama wapo,je ni mda gani tutawaruhusu kukaa nao.

Swali#15:Je? tutapata watoto na tunahitaji watoto wangapi na umuhimu wao kwetu ni upi?

Swali#16:Je tutakapopata watoto maisha yetu yatabadilika au tutaacha kazi au kupunguza kazi au tutatafuta mtu kwaajili ya malezi.

Swali#17:Je marafiki tulionao wanatosha au itakiwa tupunguze au kuongeza na faida yake ni ipi?

Swali#18:Je dini zetu ni sawa kama si sawa je mahusiano yetu yanaweza kudumu ikiwa dini zetu ni tofauti.

Swali#19:Je kila mtu ana mda wa kufanya ibada peke yake na je kila mmoja anaelewa hali ya mwenzake.

Mpenzi msomaji hayo ni maswali baadhi ambayo unapaswa kujiuliza hata kama hukuwahi jiuliza embu jitafakari kwanza huenda kama ukiyatazama kwa sasa yakawa na faida siku za usoni katika ndoa yako.

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu