Enter your keyword

Culture for Life.

Monday, August 5, 2013

Saratani ya Shingo ya Kizazi


Naamini Mpenzi Msomaji  unaye jaribu kufuatilia makala zangu za afya unanielewa vema,Pia naomba mpenzi msomaji kama unatatizo ni vema zaidi ukimuona dakitari ikiwa kile nilichokisema hapa kinakugusa kwa namna moja au nyingine, huenda ndugu,Rafiki au Jirani yako anatatizo hili ni vema umshauri kwenda  kituo cha afya mapema.Naomba kuelezea ugonjwa huu wa Saratani ya Shingo ya Kizazi kama ifuatavyo.

Saratani ya Shingo ya  Kizazi huwapata wanawake zaidi ya Laki tano kwa Mwaka ambao huwa na maambukizi ya ugonjwa huu.Zaidi ya asilimia 80 ya Wanawake hao wanaishi katika nchi masikini,zaidi ya vifo 274,000vya wanawake husababishwa na Ugonjwa huu kila Mwaka,kila baada ya dakika 2,mwanamke mmoja anafariki kutokana na Saratani ya Shingo ya kizazi duniani kote
.

Kati ya wanawake wawili wanaofariki kwa Saratani ya matiti,mmoja hufariki kwa Saratani ya Shingo ya Kizazi duniani kote,Saratani hii inashika nafasi ya pili katika Saratani za wanawake duniani.Na ndiyo sababu kubwa ya vifo vya wanawake kwenye nchi zinazoendelea.Tutambue kuwa Takwimu zilizo tajwa hapo juu sio namba tu,zinawakilisha wake zetu,mama zetu,mabinti zetu na rafiki zetu.

Dalili ya Saratani ya Shingo ya Kizazi

Saratani hutokea wakati chembe hai za sehemu yoyote ya mwili zinapokuwa bila mpangilio maalum katika shingo ya kizazi.Shingo ya Kizazi ni sehemu ya mfuko wa uzazi inayounganisha sehemu ya ndani na sehemu ya n’je (uke)

Human Papilloma Virus(HPV)

Hivi ni virusi ambavyo husababisha Saratani ya shingo ya Kizazi,Saratani ya Shingo ya Kizazi huchukua miaka 10-20 tangu kuambukizwa au mara nyingine inaweza kuchukua miaka miwili tu kutokea kwa Saratani.

Saratani ya Shingo ya Kizazi  husababishwa na vitu vifuaatavyo:


Wanawake wengi ambao hukutwa na Saratani ya Shingo ya kizazi ni kuanzia miaka
35-55,wengi wao huwa wameambukizwa na HPV wakiwa na umri kati ya miaka 13-20.

  • Kufanya tendo la ndoa katika umri mdogo
  • Upungufu wa kinga mwilini
  • Kurithishana kati ya vizazi
  • Ugonjwa wa mkanda wa Jeshi.
  • Kuzaa watoto wengi
  • Upungufu wa Madini ya Folic acid
  • Magonjwa ya ngono yanayojirudia
  • Kufanya mapenzi na mtu zaidi ya mmoja

Dalili za Saratani ya Shingo ya Kizazi

  • Kutoka kwa damu ukeni kwa hali isiyo ya kawaida kwa uzito
  • Maumivu makali wakati wa Kujamiana
  • Kuvimba kwenye kinena
  • Kutokwa na mkojo au kinyesi kusikozuilika,Pia ijulikane kuwa dalili hizi pia zinaweza kutokea katika magonjwa mengine ya Saratani ya Shingo ya kizazi,ni vizuri kupata ushauri ili ujue tatizo linalosababisha hizo dalili.
Mpenzi msomaji Mada hii nimeirejea katika kipeperushi cha
 “Tupambane Kutokomeza Saratani ya Shingo ya Kizazi”kilichotolewa na GlaxoSmithKline(GSK)kwa lengo la kuboresha afya.Asanteni

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu