Mavazi ni Sababu ya Wewe kutovutia:
By
SINYATIBLOG
On
August 21, 2013
In
Urembo
Mavazi ya Rangi Nyeusi.
| Black Gown |
Nguo Nyeusi siku zote huwapendeza
watu wengi na haichagui rangi ya ngozi ya mtu pia unaweza kuvaa nguo yenye
rangi nyeusi sehemu yoyote.Wanawake
wanaweza kuvaa nguo ya rangi hii na kuing’arisha na vikorombwezo vingine mfano
Hereni,Mkufu,Bangiri,Pochi na Viatu au Skafu. Lakini unapokosea kuvaa nguo ya
rangi hii lazima utapoteza muonekano wako ni kiwa na maana kuwa huwezi
kupendeza endapo hutapangilia vazi hili.Pia wanaume ni vema kujipangilia endapo utavaa Shati jeusi basi tambua utavaa
na suruali gani kulingana na Shati lilivyobuniwa kama linaendana na Jinsi vaa Jinsi
na kama linafaa kuvalia suruali ya kitambaa vaa hivyo pia zingatia mazingira
unayokwenda.
Usivae Nguo ambayo inakuficha sana Mwili wako.
| Pic credit.www.aliexpress.com |
Sina maana kuwa watu wavae nguo
za kuacha miili yao,ni kwamba vaa nguo ya heshima na iliyo katika mpangilio
kama fupi isidhidi magoti,pia kama ndefu iwe ndefu isiwe ya kuishia katikati ya
miguu,Kitu ninacho maanisha ni kwamba tusiwe na tabia ya kuvaa nguo nyingi kwa
wakati mmoja kiasi kwamba hueleweki umevaa nini? Na kuufanya mwili wako kuelemewa
na nguo.Usipende kuvaa vitu vizito au kiatu chenye sori ambayo ni nzito na I
kakupelekea kushindwa kutembea.
Kuvaa Brazia ambayo sio kipimo cha maziwa yako. | |
| Bra |
Ukikosea kipimo cha maziwa yako
katika kuchagua Brazia ya kuvaa,Maziwa yako yatashuka chini na kukufanya
uonekane un Maziwa makubwa, Mama anaye
nyonyesha akijua kipimo cha maziwa yake anaweza kuonekana mrembo zaidi kuliko
wewe ambaye Brazia yako imebeba maziwa.Kama hujui kipimo cha maziwa yako,jaribu
kwenda maduka ya hivyo vitu na utatambua kipimo chako.


