Enter your keyword

Culture for Life.

Wednesday, June 10, 2015

JINSI WAZAZI WANAVYO WAHARIBU WATOTO .




Uelimshaji wa mtoto ni jukumu la kila mtu.Kumbuka kuwa moja ya vitu vinavyowachanganya watoto ni makuzi ya watoto katika mazingira wanayo lelewa.Leo katika safu napenda kuzungumzia baadhi vipengele ambavyo vitamuweka mtoto wako katika mazingira mazuri ikiwa wazazi watazingatia haya katika kuwa sahihisha watoto na wakuwarekebisha.

  1. Image result for watoto

    Usahihishaji wa dhana au maneno katika kuyaelewa na kuyatamka.mfano

     

Mtoto- Mtoto anaona mtoto wa Punda kisha anamwambia mama Mbwa.Hapa wazazi wengine huitikia ndiyo Mbwa bila kujua kuwa anampotosha mtoto.Mama ilitakiwa aseme hapana  ni mtoto wa Punda.Hapo mtoto wakati mwingine hatosema Mbwa anatasema mama Punda.

  1. Urekebishaji wa tabia,kukemea na kupongeza.Mtoto mwenye tabia ya kutukana anapaswa kukemea na anapokuwa na tabia nzuri anapaswa kupongezwa.
  2. Mpangilio sahihi wa maneno.(Sintaksia ya watoto)Mara nyingi wazazi hawazingatii urekebishaji wa makosa ya kisarufi kwa watoto zaidi huzingatia maana .Kimsingi mtoto anapaswa kufundishwa namna ya kupangilia maneno katika sentensi na katika matumizi ya nyakati.Mfano.
              Mtoto- Juma ataenda shule jana.
               Mtu mzima- Juma alienda shule jana.kumbuka kuwa mtoto mdogo anauwezo mkubwa wa kujifunza lugha kuliko mtu mzima.Hivyo basi mtoto anaporekebishwa akiwa mdogo hatoweza kukosea tena.






No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu