Enter your keyword

Culture for Life.

Wednesday, September 27, 2017

Jinsi kijana unavyoweza kuchangamkia fursa katika sanaa #mimi na sanaa

Gerald Soka ni kijana  aliyemaliza shahada ya utalii katika chuo kikuu cha Dodoma Tanzania.Mbali na shahada hiyo Gerald anasema alikuwa anapenda sana kuchora na alishawahi kuwa mshindi katika uchoraji kipindi cha UMITASHUNTA mwaka 1999.Anasema baada ya kumaliza chuo alipata nafasi ya kutembelea Uganda na rafiki yake.

Saa ya ukutani

Gerald Anasema alipofika Uganda ndipo aliona fursa ya uchoraji kuwa ni sanaa itakayomlipa.Anasema aliona kuwa vitu ambavyo jamii inaona kama uchafu lakini yeye anatumia kujiingizia kipato hasa anapo tumia katika sanaa yake.


Flame za picha

Gerald anatumia.magunia,majani ya migomba na maboksi au makaratasi na vitenge kutengenezea vitu kama.
Saa ya ukutani zenye picha iliyochorwa,flame za picha,keyholder,tablemats, menu file,tissue boksi,boksi La zawadi,lampholder,flower vessel na tissue box.

Flower vessels

Tissues boksi


Lampholdets


 FAIDA
kijana Gerald Anasema kupitia sanaa hii ya uchoraji anamsomesha mtoto,anapata mshitaji ya familia,na kuweza kulipia gharama za malazi.mbali na hayo Gerald Anasema kwa mwezi huweza kuingiza kiasi cha milioni moja endapo anatapata oda nyingi na laki nne endapo biashara haipo vizuri.Pia nimefanya kazi na kampuni kama,Africafe,Eng'noto,Triple A,nk.

CHANGAMOTO
Kwanza ni uhaba wa masoko,mtaji was kutosha,hali ya hewa hasa kipindi cha mvua migomba huwa hadimu(majani makavu).

USHAURI KWA VIJANA
Waache kubweteka,wasiwe wavivu katika kutafuta kipato wafanye kazi kwa bidii pia wajitunze.
Ukihitaji kazi za Gerald wasiliana naye kwa namba.0757746506
 email:Gerald soka@gmail.com

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu