Enter your keyword

Culture for Life.

Sunday, December 18, 2016

JINSI YA KUVAA JUMPSUIT

  JUMPSUIT(Bwelasuti) na uvaaji wake.

Mpenzi msomaji wa safu hii ya urembo na mitindo ya mavazi leo nataka kuwajuza historia ya vazi hili ambalo kwa sasa limekuwa likivaliwa sana katika mandhari mbalimbali.

Mtindo huu Jumpsuit unaweza ubadilisha badala ya kuvalia suruali pia unaweza kuvaa na skirt fupi au kigauni kifupi na high heels.

Bwela suti au ovaroli(Jumpsuit) mwaka 1960 ni vazi ambalo zamani lilitumika sana na watu wanaoruka na parachuti kwa lengo la kuzuia hali ya baridi na upepo.

Mwaka 1987 vazi hili lilipata umaarufu katika sekta mbalimbali ambapo lilianza kuvaliwa na Marubani,madereva,wanamichezo,Mafundi bomba,mafundi mitambo,Wasanii  pia huvaa jukwaani, huku vyuoni/mashuleni  likivaliwa kama sale katika vyuo vya ufundi.

Wazazi wengi huwavalisha bwelasuti watoto  wanaotambaa kwa lengo la kuzuia baridi pia kuhofia  kuchafuka kwa wale walio katika kipindi cha kutambaa.

Hicho kibwebwe cha nyuma waweza shona kwa style ya kukitoa,unakuwa na uwezo wa kuivaa nguo moja katika muonekano tofauti.

Vazi hili limeendelea kushika nafasi kubwa katika swala la mitindo huku wabunifu wengi  wakibuni vazi hili katika mitindo mbalimbali.
Jinsi ya kuvaa bwela suti

1.Tambua kiuno chako
Hakikisha unajua kipimo cha kiuno chako wakati wa kuchagua bwelasuti iliyo sahihi.Lazima rastiki au mkanda  uliopo katika bwela suti ushike vema kiuno chako ili kuepusha muonekano mbaya wa umbile lako .

2.Fanya chaguo sahihi la bwela suti kulingana na umbo lako
Nivema kutambua umbo lako ili kuweza kuonekana nadhifu ndani ya vazi hili.Kwanza kabisa kwa wale wenye miguu mrefu ni vema kuvaa bwela suti ambazo ni pana miguuni,watu wafupi au wenye urefu wa wastani hutakiwa kuangalia aina ya kitambaa na urefu wa vazi hili.

Wenye maziwa madogo,mikono miyembamba lakini wamejariwa nyonga(hips) unatakiwa kuvaa bwela suti yenye muonekano wa blauzi zaidi pia iweze kuonyesha  mikono yako vizuri.hii itazuia muonekano wa nyonga zako zaidi.

3.Vaa bwela suti na koti
Watu wengi huofia kuvaa bwela suti kutoka na mitindo mbalimbali ya vazi hili kuonyesha mabega,mgongo na sehemu kubwa ya mikono.Kama wewe ni mmoja wapo jaribu kuvaa vazi hili na koti,utaonekana nadhifu pia litakuzuia baridi na kuficha mikono yako  ni vema koti liwe fupi ili kuonyesha umbo lako na mtindo wa bwela suti uliyoivaa..

4.Uchaguzi wa rangi za bwela suti
Bwela suti yenye rangi moja huvutia zaidi kuliko bwela suti yenye rangi moja juu na chini rangi nyingine au yenye mchanganyiko wa rangi mbalimbali chini,Katika uchaguzi wa rangi wengi hutofautiana kulingana na chaguo la mvaaji.

5.Uchaguzi wa kiatu cha kuvalia bwela suti
Unaweza kuvaa viatu vya chini(Flat shoes) au viatu virefu na bado ukaonekana  mwanamke nadhifu na mwenye kuvutia zaidi bila kujali umri ulionao wala umbo lako.

Vazi hili  huweza kuvaliwa nyakati zote na katika matukio tofauti, kitu cha msingi mvaaji aangalie mtindo wa bwela suti ,aina ya kitambaa na eneo analokwenda na tukio(sherehe).

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu