Enter your keyword

Culture for Life.

Saturday, January 19, 2013

Bongo flava na historia yake

Historia fupi ya muziki wa kizazi kipya
  ulianzishwa na Wamerekani weusi huko the Bronx, New York Marekani mnamo mwaka 1970.Wamerekani wenye asili ya Afrika ,ambao babu zao walichukuliwa kwenda Marekani kama watumwa.Elementi hizi za utamaduni wa hiphop zilikuwa zikijitokeza kwa awamu moja  na inapofifia inaibuka nyingine ,ilivyo ni kwamba ilianza grafiti ikafuatwa na udijei,mabreka,halafu rap(yasin,2001;rose1994;toop2000;mitchel2001;southern1983).
Mizizi hasa ya rap Afrika, mbali ya kuanzishwa na wamarekani weusi una sifa mbalimbali za kimuziki na kifasihi simulizi za kiafrika ikiwa ni pamoja na matumizi ya midundo au ridhimu usimulizi,kiitikio na majigambo.Hiphop au muziki wa kizazi kipya ulikuwa kama jukwaa la mshikamano miongoni mwa vijana wa kimarekani  wa mjini na baadaye kuwa kama mtindo  wa maisha na sauti ya vijana .Ni utamaduni ambao uliwakutanisha wale walionyimwa haki ,walionyanyaswa  na kugandamizwa katika historia  na ukawa utambulisho  miongoni mwa Wamerekani weusi na ukawa kipaza sauti chao.

Muziki wa kizazi kipya au rap nikipengele kimoja wapo  cha utamaduni wa hiphop.Ni aina ya ushairi ,usimuliaji,au usemaji unaopangwa vina kwa kufuata mdundo wa ala  za muziki (ambao tayari ulisharekodiwa ).Muziki huu ulianza kama sehemu ya burudani  ya vijana weusi na baadaye  ukakuwa na kuenea  na kuwa maarufu  katika nchi nyingi  duniani .Hapa Tanzania  muziki wa kizazi kipya ulianza mwaka 1980.Vijana walianza  kuimba wakiwa ufukweni na baadaye katika sherehe mbalimbali ulianza kisikika redioni  mwaka 1995.
Kama ilivyokuwa kwa Wamerekani weusi vijana wengi  wa Kitanzania pia hutumia muziki wa kizazi kipya  kuelezea matatizo yao  ya kila siku kama vile ukosefu wa ajira  na athari zake ,Dola na nguvu zake  na umasikini.Hapo mwanzoni  nyimbo hizi ziliimbwa kwa kuwaiga wasanii wa  kimarekani  kama vile Vanillah Ice,Kriss Kross na Naughty by Nature, halikadhalika walitumia  baadhi ya maneno au sentensi kutoka nyimbo hizo .Hivyo kila mwimbaji  alijaribu kuwa mbunifu na kutunga nyimbo zake mwenyewe ilikuwapata mashabiki na kujiongezea umaarufu.Muziki wa kizazi kipya unaojulikana sana kwa jina la Bongo flava ulishika kasi sana mwaka2000.muziki huu umewapatia vijana wengi  fusra baada ya kusikia nyimbo kutoka n’je ya

Tanzania  hususani marekani ambapo vijana waliiga na kutoka na staili yao wakitumia lugha ya Kiswahili na wengine walichanganya nyimbo hizo na lugha kama Kingereza na lugha za asili.
Walichoweza kufanya vijana wengi ni kuiga (ala) za Wamerekani lakini waliamua kutumia lugha ya Kiswahili ili kuweza kufikisha ujumbe  kwa Watanzani na kama inavyojulikana kuwa kazi yoyote ya sanaa ina malengo  ya kufundisha ,kukosoa na kuburudisha.Wakati muziki huu unaanza Tanzania  hakuweza kuzaniwa kama unge fika karne za mbele lakini hivi sasa una waimbaji wengi pamoja na mashabiki wengi wa rika tofauti hasa vijana, watu wazima si wote wanao upenda muziki huu.
Baadhi ya vijana waliokuwa waanzilishi wa muziki huu kwa Tanzania,vijana wa mwanzo kabisa ambao kuanzia mavazi yao na kufokafoka kwao kulikuwa ni burudani tosha kwa watu kuanza kudadisi kuhusu utamaduni wa mavazi hayo ambayo yalionekana  kama uhuni tena wa kupita kiasi kutokana na uvaaji wa mavazi hayo kihip hop.Hawa ni baadhi ya wasanii wachache ambao walivaa kihip hop Samora Avenue,John simple,DJ Rusual,The BIG ONE,Babu manju,Davidi,Nhigula,Abdulhakim Magomelo,Kessy,Ibony Moalim,Tom
 London,Opp(now JayP)  NA DJ Ngomeley.Hao walikuwa chachu katika uvaaji wa kihiphop na katika kughani Muziki huu wa kizazi kipya.
Pia kuna wasanii wa mwanzo kabisa katika kuimba muziki huu wa kizazimkipya akiwepo mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi (BBG lianza na MR.11)FreshXE Mtui,Adili Kumbuka,KBC(Mbeya Tech)Saleh Jabir,Samia X,The Big,Rhymson,2Proud,Kwanza Unit,GWM,Hard Blasters na Bantu pound ambao walianza kuimba katika sherehe za mashuleni,kwenye matamasha mtaani kabla hata ya kurekodi nyimbo zao studio. Kulikuwa na wale wenye kuimba kama wanamuziki wengi wa Marekani kwa kupitia matamasha mbali mbali katika Jumba la utamaduni la Urusi,Korea na mengineyo yaliyokuwa yakiandaliwa hasa na wanafunzi wa shule mbali mbali za sekondari jijini kama Forodhani pia matamasha yaliyokuwa yakifanyika kando kando ya ufukwe ambako wengi wenye kutaka kuimba walijitokeza.

Kulikuwa na  kundi kama la Mawingu na mwana dada Pamela,mwanadada Stara Thomas na Judith Wambura ambao uwezo wa kughani na kuimba kama Mc Lyte ulimuinua hasa alipofanya hivyo kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha DJ show ya Radio One,shukrani kwa Ipyana Malecela Mkwavi (RIP) kwa zawadi ya LP yenye mdundo,ala ya single “Keep,Keeping on” ndiyo iliyomtambulisha Jay Dee wa leo Radioni kwa mara ya kwanza japokuwa kabla ya hapo alikuwa mwimbaji wa kwaya kanisani lakini mweye kusita kuingia kwenye muziki wa kidunia.
Pia Kundi la R&B lililojulikana kama Four Krewz Flava pia Herbert Makange ambaye pia alikuwa akiimba. Kwa kufanya haya na mengineyo mengi muziki huu sio tu utakuwa ni wenye kujijengea heshima bali kuweka kumbukumbu kubwa ya mapinduzi kwenye ulimwengu wa muziki Tanzania na hadhi yake kuwa ni ile isiyofutika kwa urahisi machoni na akilini mwa kizazi cha sasa na hata kile kijacho kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu