Enter your keyword

Culture for Life.

Saturday, December 15, 2012

Vitu vya Msingi kwenye mkoba wa mwanamke

Vitu vya msingi  kwa mwanamke katika  Mkoba(Hand bag )wako.
Naomba leo tukumbushane mambo matano ambayo yanaweza kuwa msaada kwetu.Wanawake tunamambo mengi na wakati mwingine tunaweza kushau mambo ya msingi kutokana na kutokuwa na mpangilio mzuri,
Hivyo basi ilikuondokana na tabia hii ni vema leo katika safu yetu ya Urembo na mitindo tukumbushane mambo hayo matano:
Pochi
Ni muhimu kuwa na pochi ndani ya mkoba wako ambayo itakuwa na pesa,kadi ya benki,vitambulisho na vitu vingine ambavyo unaweza uka weka katika pochi yako.Hii itakusaidia kujua vitu kama hivyo vipo sehemu gani katika pochi yako  kuliko kufungua mkoba mzima na kuanza kutafuta.
Simu
Nafahamu kuwa ni vigumu kutembea bila simu hivyo basi chagua sehemu maalumu ambayo utakuwa unaiweka simu yako  hasa katika mifuko ya ndani ya Mkoba , ilikuhakikisha  kuwa usahau sehemu ulio weka na kuondoa usumbufu wa kukagua begi zima simu itakapoita au wakati ukihitaji kuitumia.
Funguo
Tusisahau funguo maana utakapoteza itakufanya uzunguke siku nzima kutafuta hasa sehemu ulizo pita katika mizunguko yako na  huu msururu wa magari  barabarani utakufanya uchanganyikiwe zaidi.
Kipochi kidogo
Ni  vema ukiwa na kipochi kidogo  kwa ajili ya kuwekea vitu kama rangi za midomo(lipstics),wanja,poda,mafuta,vitana,ilikuzuia mpangilio mbaya wa vitu ndani ya mkoba wako pia kuzuia kuchafua mkoba endapo vikimwagika .
Daftari(Notebook) na kalaamu
Litakusaidia kujua vitu unavyohitaji kununua na pia utaweza kuorodhesha vitu ulivyo nunua,kwa wale wenye tabia ya kusahau vitu  alivyopangilia kuvifanya mahali anapo kwenda  na hukumbuka wakati amekwisha rudi nyumbani nadhani daftari ni la msingi sana kwao.

Kanga
Mwanamke  lazima utembee na kanga au kitenge mda wote kiwe ndani ya mkoba wako ili usihadhirike unapopatwa na tatizo.Hapa inategemea unaelekea wapi? Usije ukabeba kanga au kitenge wakati unakwenda kwenye sherehe.Unapokuwa na safari ndefu ni muhimu kubeba kanga.Kama haitakusaidia wewe itamsaidia mtu mwingine.
Viatu (Flatshoose)
Hasa wanaopenda  kuvaa viatu virefu na hata wengine kwa ajili ya tahadhari pale kiatu kinapokuwa kimekatika kitakusaidia kulinda unadhifu wako na kuepusha aibu.Nimetaja vitu vichache lakini kuna vile vingine ambavyo ni muhimu kwa mwanamke hasa ukishajua nyakati zako,nimekuwa nikishuhudia wanawake wengi wakipatwa na aibu kutokana na hilo tuwe makini.
0756377940.

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu