Enter your keyword

Culture for Life.

Tuesday, February 26, 2013

False eyeleshes(Namna ya kutumia kope bandia)



kope bandia

jicho ambalo lisha valishwa kope bandia

Gundi ya kope bandia
Watu wengi hupenda kope ndefu na kulazimika kutumia kope bandia hasa wenye kope fupi na wale wenye macho madogo,Unapotumia kope bandia hufanya macho yako yaonekane vizuri na yavutie zaidi.Vitu utavyohitaji kabla ya kuweka kope bandia ni :Kope bandia zenyewe, gundi ya kope bandia(False eyelash glue)Maskara na kioo.Njia ambazo zitakusaidia wakati wa kuweka kope bandia hasa  ambao hawapendi kwenda saluni na wana uwezo wa kuweka wenyewe.

1.Chagua kipimo sahihi cha kope bandia.kabla ya kuweka Gundi katika kope hakikishaumechagua urefu sahihi wa kope unazohitaji,pia acha Gundi ikauke kwanza kidogo kisha bandika kope zako,acha iendelee kukauka yenyewe pia usiishikilie wala kukandamiza ili kope zishike vizuri usifanye hivyo ukimaliza kubandika achia na zitaendelea kukauka zenyewe.
    
2.Tumia maskara (mascara)  kwenye kope bandia,ukipaka maskara kwenye kope zako zitazifanya zionekane asilia,unaweza kutumia maskara rangi nyeusi na blauni.


3.Tumia wanja wa maji,unaweza kuupaka kwenye mstari wa kope ya juu ili kuficha uwazi uliopo baada ya kuweka kope bandia  pia unaweza kutumia wanja mweusi au blauni kulingana na na ngozi yako na wanja unaopendelea kuutumia.

4.Tumia kitu cha maji maji(makeup remover)ambacho husadia kuondoa kope bandia kwa urahisi zaidi,baada ya hapo unaweza kutoa taratibu kope zako.

Zingatia:
Hakikisha unazisafisha vizuri hizo kope na kuziweka mahali salamakama unampango wa kuzitumia tena.
Tumia kitu cha maji maji kuzisafisha(makeup remover)ili kuweza kuondoa maskara pamoja na wanja 
Hakikisha unaondoa kope bandia kabla ya kwenda kulala
Usipende kuchangia kope bandia na mtu yeyote wala vipodozi vya usoni ilikuepuka maambukizi yasiyo na tija
Endapo gundi itaingia kwenye macho hakikisha unaosha haraka na maji ya moto kiasi au uvuguvugu.
Pia ni muhimu kuosha mikono yako kabla hujaanza kuweka kopebandia

Mwisho kabisa mpenzi msomaji wa safu hii hakikisha unatumia kope hizi za bandia vema nikiwa na maana kwamba kuna kope zingine ni za rangi.Itakuwa ajabu mtu atakapo tumia kope za rangi wakati anaelekea kanisani,sababu utafanya watu wote wawe wana kutazama wewe,tumia kope bandia lakini zingatia mandhari unayokwenda.Usisite kunitumia maoni kupitia namba yangu ya simu kwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno au barua pepe.
abnerytupokigwe@gmail.com ,   0756 377940
      

   

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu