Enter your keyword

Culture for Life.

Thursday, April 6, 2017

Sifa za malikia wa nguvu katika muoenekano wa mavazi.

 

Anne Kansiime. Kansiime Kubiryaba Anne (amezaliwa 13 April 1987) anajulikana kwa jina la umaarufu Anne Kansiime ni msanii wa vichekesho kutoka uganda watu hupenda kumwita malikia wa afrika katika vichekesho.Ni mwanamke ninaye mkubali katika tasnia ya usanii na huwa anapenda kuwa kiafrica rangi ya ngozi yake ni kivutio tosha kama mwanamke wa kiafrika.


Kuna msemo usemao kuwa “mwanamke ni pambo la nyumba”hivyo basi kama mwanamke ni pambo la nyumba ndani hata n’je pia  unastahili kuwa nadhifu.Leo katika safu hii ya urembo na mitindo nitazungumzia vitu vichache ambavyo vitakusaidia wewe mwanamke bila kujali kipato chako cha uchumi.

Kujiamini na kujikubali 

 wanawake wengi hushindwa kuvaa baadhi ya mavazi kutokana na maumbile yao,Huona  kuwa miili  yao haiwezi kupendeza katika  mavazi mengine.Mfano wapo watu ambao hushindwa kuvaa nguo fupi kutokana na kuona kuwa miguu yao ni mibaya.Unapaswa kuujua mwili wako  na  mavazi ambayo yanakupendeza na kukuonyesha nadhifu,kwa watu wanene ni vema kuvaa nguo ambazo nipana nikiwa na maana kuwa zisichore mwili wako na kutengeneza muonekano mbaya.Wale wembamba wao wana uhuru katika mavazi isipokuwa usipo jitambua utaonekana kituko uchaguzi wa vazi utakalo kuwa umevaa.

Tambua rangi ya nguo zinazokupendeza,

 

Yvonne Chaka Chaka is My Second Mom — Anne Kansiime

chagua rangi inayoendana na ngozi yako ambayo itakuonyesha vema,kuna baadhi ya rangi ukivaa zitakufifisha  na kukufanya uonekane ujapendeza hata kama vazi lako ni zuri na la thamani.

Panga bajeti  

kwaajili ya kununua vitu vyako vya msingi ni kimaanisha mavazi,heleni.bangili,mkufu,Hapa mwanamke unashauriwa kununua gauni jeusi,katika manunuzi yako, gauni jeusi fupi au refu,hili litakusaidia unapokuwa na mtoko au sherehe utaweza kutupia gauni lako na kuchanganya na heleni bangili au mikufu na utaweza kuvaa kwenye  mtukio tofauti na kuoneka mpya huku uikiwa umeficha umasikini.

Fanya mazoezi

wanawake wengi hatuna kasumba ya kufanya mazoezi siku zote.Maozezi ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha viungo vyetu na kutengeneza muonekano wa mwili(body shape).Hii itakusaidia kuepuka matumizi ya dawa zakuongeza maumbile mfano dawa za kuongeza nyonga(hips) na makalio. 

Tumia Maji na Matunda 

ni muhimu kunywa maji angalau lita moja kwa siku kiafya,itakusaidia kuimnarisha ngozi yako,pia jitahidi kupata matunda katika mlo wako au unaweza kutumia matunda kama kifungua kinywa chako na kuepuka utumiaji wa vitafunwa vyenye mafuta.
  

Epuka utumiaji wa madawa ya kongeza maumbile,

 kubadilisha ngozi nikiwa na maana ya vipodozi vya kuchubua mfano Carolight.Hivyo ni baadhi vitu vichache ambavyo ukizingatia mwanamke utaendelea kuonekana kijana na kuepuka uzee usio wa lazima naomba mchunguze watu wengi wamepata madhara baada ya kutumia dawa hizi.Utazifurahia kwa mda mfupi lakini madhara yake ni makubwa. 

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu