Enter your keyword

Culture for Life.

Thursday, December 15, 2016

The Rise Of African Queen and King."Mwanamke Akiwezeshwa Anaweza"


Tangu Juma lililopita Makeke na Studio Maisha  tumeshirikiana kuandaaa project Mpya na tayari awamu ya kwanza imefanyika na imeonekana kukubalika zaidi kwa jamii na wadau wa mitindo, project inaitwa THE RISE OF AFRICAN QUEEN

Jocktan Makeke alisema  hasa Katika mahojiano aliyofanya na Sinyatiblog siku ya trh 13/12/2016”
Jocktan alisema”Kuna kauli isemayo mwanamke akiwezeshwa anaweza, kama ilivo kauli hio project hii imejikita zaidi kumsaidia mwanamke hasa  mwanamke mwenye ndoto ya kuwa mwanamitindo wa kimataifa, Wazo hili lilikuja baada ya kuona kuwa wapo wanawake wengi sana wenye  vipaji na wana vigezo vyote vya kuwa wanamitindo bora wa hapo badaye lakini wana kosa msaada kuhusu wapi wataanzia na watafikaje? Kiwango  cha  kimataifa katika masuala ya mitindo.

Project hii inahusu wasichana wenye  umri kuanzia  miaka 18 hadi 22.Waandaaji wa Project hii  ni MAISHA STUDIO kampuni inayojihusisha na masuala ya upigaji wa Picha , na MAKEKE AFRIKA  kampuni ya mitindo ya kiasili.


Kwa kila  mwezi  mmoja tutakuwa tukiwatoa watu wawili  ambao ni new faces, project hii imeanza na wasichana kwanza lakini hapo badaye tutaendelea na THE RISE OF AFRICAN KINGS ambayo itakuwa kwa vijana wa kiume tu na mwisho tutamaliza na THE RISE OF AFFICAN KING & QUEEN hapo tutajumuisha vijana wawili kila mwezi, wa kike na wa kiume.

Tunaamini kuwa project hii itakuwa ni fursa na mlango Mpya kwa vijana kwani hawatagharamika kwa kitu chochote na Picha zao zitasambazwa kwenye media  zetu mbalimbali , pia vijana kushiriliki majukwaa mbaimbali ya mitindo , kitaifa na kimataifa.
Sinyatiblog:hongera kazi nzuri na mchango wenu  ni mkubwa sana kwa jamii,je mnatarajia kushirikisha mikoa yote au ni Dar tu je taratibu zikoje kwa mtu anayetaka kushiriki.
Jocktan: Hatulipani chochote kwasababu  ni kwaajili yao, ukisema sasa  hivi  umchukue mpiga picha mkali umpeleke eneo la kupigia picha, ni Pesa nyingi sana ambazo ni ngumu
kugharamia,Kwahiyo kupitia project itakuwa bure tu na kwasasa tunaanzia Dar tu baadaye ndiyo tutafika mikoani.Vilevile Wana mitindo tumaozungumzia hapa ni modelz tu.Kwasasa tumeanza tayari na Models wawili.

 Hao ni models ambao wamekwisha anza kufanya hii project ya The Rise of African Qeen.


No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu