Enter your keyword

Culture for Life.

Thursday, December 15, 2016

Vazi la kitenge litumike katika Sherehe zote za kitaifa."Maoni Ya Neema Daniel"




Neema Daniel ni mjasiriamali anayejishughulisha na ubunifu wa vitu vya asili kwa kutumia vitenge.Anabuni viatu na mikoba ya vitenge.


Kitengeflat shoes

Mahojiano ya Neema na Sinyatiblog yaliyofanyika  kwa njia ya Whatsapp na Facebook messenger.

 

 Sinyatiblog:Neema unajishughulisha na nini ili kupambana na maisha.

Sinyatiblog:Nauza vitenge,nashona nguo za vitenge ,natengeneza viatu na handbag za vitenge.

Neema:Wateja wangu wengi ni wafanyakazi wa maofisini na kwenye mitandao.
Sinyatiblog:Nini kinafanya kazi zako zionekane ni za tofauti na kazi za wengine?
Neema:Utofauti wangu ni kwamba watu wamezoea kubeba handbag za ngozi,mimi nimeibadilisha kidogo kwa kuivalisha kitenge na kiatu pia, sasa imekuwa tofauti na inavutia wengi.





Sinyatiblog:Unatumia material gani hasa katika kutengeneza hizo handbag na viatu.
Neema: Huwa nanunua handbag au viatu alafu naivalisha kitenge.
Makenzi flat shoes na Mkoba.Unaweza kuvaa na nguo ya rangi moja pamoja na kujipamba kwa nakshi kama bangili mkufu na hereni.

Sinyatiblog:unaishauri nini jamii kuhusiana na kupenda vitu vya asili hasa vya ndani ya nchi.
Neema:Nashauri jamii wapende vitu  vya asili maana ndiyo asili yetu kwa afrika

Sinyatiblog:Neno  moja kwa jamii unaloweza kuwashauri.
Neema:Okay tupende kuwa wabunifu wa vitu mbalimbali ili isaidie kuongeza kipato.
Sinyatiblog:kama ungepata fursa ya kushauri serikali  kuhusu vazi la  taifa ungesemaje?
Neema:Ningependeza sana kila sherehe za kitaifa kuwe na sare za vitenge kama vazi letu la kitaifa.

Hii ni raba ya kawaida lakini imevalishiwa kitenge na kibao kwaajili ya mtoto.


Mawasiliano ya Neema Daniel.
Napatikana insta:Ulimwengu_wa_vitenge.
No.0713655363
DSM-Kigamboni

No comments:

Post a Comment

3 Bora Zangu

Inayotazamwa Sana

Jinsi Ya Kuufanikisha Mwaka 2017

Mpenzi msomaji wa Makala zangu kwanza kabisa nachukua fursa hii kuwashukuru wote mnaofuatilia Blog yangu,Naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya...

Watazamaji Wangu